

Maembe hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Tabora, Pwani, Mtwara, Tanga, Mwanza, Morogoro na Mbeya. Uzalishaji wake ni wastani wa tani 159,472 kwa mwaka. Maembe ni zao muhimu la biashara na chakula.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UZALISHAJI
Ili kupata mazao bora ni muhimu kuzingatia kanuni bora za kilimo cha maembe hasa kanuni
zifuatazo:
Kuchagua aina bora ya kupanda kulingana na mahitaji ya soko.
Panda umbali wa mita 10 kwa kumi kama utatumia miembe ya kuunga, hii ni kwa sababu haiwi mikubwa sana kwa sababu haiishi miaka mingi, kwa ile ambayo si ya kuunga panda umbali wa mita 15 kwa 15 kwa kila mti mmoja wa muembe
DHIBITI MAGONJWA, WADUDU, NA MAGUGU
• Fanya ukaguzi wa shamba mara kwa mara ili uweze kudhibiti wadudu na magonjwa ya matunda kabla madhara hayajawa makubwa
UGONJWA WA KUTU KWENYE MAJANI

• Ni muhimu kudhibiti wadudu, magonjwa na magugu ili kupata mazao bora ambayo yatapata soko zuri na kuweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
• Hakikisha shamba ni safi wakati wote ili kupata matunda bora na kurahisisha uvunaji.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA
Kusafisha shamba pamoja na barabara za shamba
• Safisha shamba ili kurahisisha uvunaji na usafirishaji shambani.
Kukagua shamba kuona maembe kama yamekomaa Maembe hukomaa katika kipindi cha miezi 4 hadi-6 tangu kutoa maua kutegemea hali ya hewa na aina.
DALILI ZA MAEMBE YALIYOKOMAA
• Maembe hung’ara
• Kwa aina nyingine rangi ya kijani hufifia na kuanza kubadilika kuwa ya manjano.
ANDAA VIFAA VYA KUBEBEA, SEHEMU YA KUFUNGASHIA NA USAFIRI.
VIFAA VYA KUBEBEA
• Ngazi
• Vikapu
• Mifuko
• Ndoo
• Vichumio
VIFAA VYA KUFUNGASHIA
• Makasha ya mbao/plastiki na ya makaratasi magumu na matenga
VYOMBO VYA KUSAFIRISHIA
• Matoroli
• Magari
• Baiskeli
• Matela ya matrekta
KUVUNA
Njia bora ya kuvuna maembe ni Kuchuma kwa mkono
• Kwa miembe mifupi chuma maembe pamoja na kikonyo chake
• Kwa miembe mirefu chuma kwa kutumia kichumio maalumu
KICHUMIO MAALUM

• Acha kikonyo chenye urefu wa sentimita tatu hadi nne ili kuzuia madoa ya utomvu. Utomvu huchafua matunda na hushusha ubora. Pia embe lililovunwa bila kikonyo chake huingiliwa na vimelea vya ugonjwa kwa urahisi.
• Vuna wakati wa asubuhi au jioni ili kuepuka jua kali linaloweza kubabua matunda.
• Wakati wa kuvuna hakikisha maembe hayadondoshwi chini, ili kuepuka kuchubuka kwa matunda ama kupondeka hasa yale yaliyoiva barabara. Aidha beba matunda kwa vikapu au mifuko na kusanya kwenye kivuli.

KUCHAMBUA MAEMBE
Kuchambua ni kutenga matunda yaliyooza, kupasuka, yenye dalili za magonjwa au kubonyea, ili kupata matunda yenye ubora kwa ajili ya matumizi, kusindika au kuuza.
• Matunda yaliyooza na yenye wadudu ni vyema yafukiwe ili kuzuia kuenea kwa wadudu waharibifu na vimelea vya magonjwa.
• Matunda yaliyopasuka, kubonyea , kuchubuka kidogo wakati wa kuvuna au kuiva sana yatumike haraka kwa chakula.
• Matunda mazuri ambayo hayajapata madhara yoyote yatunzwe kwa ajili ya kusindikwa, kutumika au kuuzwa.
KUSAFISHA MAEMBE
• Baada ya kuchambua, safisha matunda kwa maji safi ili kuondoa uchafu na mabaki ya madawa.
• Maembe yanayokusudiwa kuuzwa nje ya nchi hunyunyiziwa nta ili kuzuia kunyauka na kudumisha ubora.
• Baada ya kusafisha tumbukiza maembe kwenye maji yenye nyuzi joto zipatazo 52 za Sentigredi kwa muda wa dakika tano. Maji haya pia yanaweza kuchanganywa na madawa ya klorini asilimia 1 ili kuzuia magonjwa ya ukungu.
KUPANGA MADARAJA
Madaraja hupangwa kwa lengo la kurahisisha ufungashaji, usafirishaji na uuzaji. Madaraja hupangwa kulingana na ubora, ukubwa , aina rangi na uivaji.
KUFUNGASHA MAEMBE
Ufungashaji hufanyika katika sehemu safi na yenye kivuli. Ufungashaji wa kujaza kupita kiasi husababisha upotevu wa maembe. Aidha ubora hushuka kutokana na kuminyana na kubonyea kwa matunda wakati wa kusafirisha
TENGA LA KUFUNGASHIA MAEMBE

Inashauriwa kufungasha kwenye makasha ya mbao/ plastiki , makaratasi magumu au tenga kwa sababu zifuatazo:
• Matunda yanaweza kupangwa na kusafirishwa bila kuchubuka, kubonyea au kupasuka.
• Huweza kupakiwa na kupakuliwa kwenye chombo cha usafiri kwa urahisi.
Wakati wa ufungashaji ni muhimu kuzingatia yafuatayo:
• Kasha moja lisizidi uzito wa kilo 20 ili kurahisisha ubebaji.
• Makasha yawe imara na yenye matundu ya kutosha ili kuruhusu mzunguko wa hewa.
• Ni muhimu kutanguliza vitu vilivyo safi ndani ya vifungashio ili kuzuia michubuko na mipasuko ya matunda wakati wa kusafirisha.
• Maembe yapangwe kwa kubananisha na kwa kuhakikisha kuwa vikonyo havitoboi matunda na kusababisha majeraha wakati wa kusafirisha. Kubananisha matunda husaidia kuzuia mgongano unaoweza kusababisha matunda kusambaratika na hivyo kubonyea au kupasuka wakati wa kusafirisha.
KUSAFIRISHA
Ili kuepuka upotevu na uharibifu wakati wa kusafirisha, ni muhimu maembe yapangwe kwenye vyombo vya kufungashia na kusafirisha kwa uangalifu, ndani ya matela, mikokoteni na magari. Epuka kutupa matunda wakati wa kupakia na kupakua. Wakati wa kupanga mazao katika vyombo vya usafiri yasirundikwe ovyo na yasijazwe kupita kiasi ili yasimwagike. Vilevile yafunikwe ili yasipigwe na jua. Jua huongeza kasi ya kuoza. Matunda yakipigwa na jua kwa muda wa saa mbili mfululizo husababisha kuoza kwa asilimia 100.
KUHIFADHI
• Maembe huweza kuhifadhiwa kwenye chumba chenye hali ya hewa yenye joto la nyuzi 8 hadi 10 za Sentigredi na unyevu wa asilimia 85 hadi 90. Katika hali hiyo, maembe yanaweza kuhifadhiwa bila kuharibika kwa mwezi mmoja.
• Kagua mara kwa mara ili kugundua uharibifu unaoweza kutokea
Continue »

Maandalizi sahihi ya shamba ni jambo la msingi katika kuboresha kilimo cha umwagiliaji wa mpunga. shamba lisipoandaliwa vema husababisha mbinu bora zinazoshauriwa kutoonyesha matokeo katika kiwango kinachotarajiwa hasa katika uzalishaji. Kimsingi maandalizi ya shamba yanatakiwa yafanyike kwa usahihi
na kwa wakati katika mtiririko unaotakiwa. Zifuatazo ni hatua saba muhimu na za msingi katika kilimo cha mpunga
1. KUSAFISHA SHAMBA
Safisha shamba mapema kabla ya msimu kuanza. Kusanya na kuangamiza visiki na takataka nyingine zote. Masalia ya mazao yanaweza kutumika kutengeneza mbolea ya mboji. Inapobidi tumia moto kwa uangalifu sana maana moto unaweza kuharibu mazingira, unaua wadudu rafiki, unaharibu udongo na kuteketeza mboji.
2. KULIMA
Kulima husaidia kupunguza kiasi cha magugu, huruhusu mzunguko mzuri wa hewa na maji, hurahisisha mizizi kupenya na kuchanganya masalia ya mazao kwenye ardhi. Wakati wa kulima uangalifu unahitajika ili kuzuia kuharibu usawa wa ardhi. Kina cha kulima kiwe kati ya sentimeta 10 na 15. Ili kurahisisha na kuharakisha kazi ya kulima ni vema kutumia zana/mashine rahisi kama Trekta la mkono na wanyamakazi
3. KUKARABATI/KUJENGA MAJARUBA
Baada ya kulima hakikisha kuwa kingo za jaruba zimekarabatiwa ili kuweza kuhifadhi maji vema. Kama ni shamba jipya, ujenzi wa kingo za jaruba ufanyike kwa kufuata utaalamu unaotolewa. Kingo imara ni muhimu kudhibiti vema maji shambani.
4. KUVURUGA
Weka maji shambani kiasi cha sentimeta 3 hadi 5 juu ya usawa wa ardhi ili kukamilisha vema uvurugaji. Jembe la mkono linatumika lakini ili kurahisisha na kuharakisha kazi hii ni vema kutumia trekta la mkono au wanyamakazi. Unapotumia wanyamakazi au trekta la mkono weka maji shambani si zaidi ya siku moja kabla. Shamba lililovurugwa vema huiwezesha mizizi ya miche kupenya vema ardhini.
5. KUSAWAZISHA SHAMBA
Baada ya kuvuruga ni lazima kuhakikisha kwamba shamba limesawazishwa vema. Shamba lililosawazishwa vema linaruhusu usambaaji mzuri wa maji. Wakati wa kusawazisha kina cha maji kiwe kiasi cha sentimeta 3-5 juu ya usawa wa ardhi Ili kurahisha kazi hii tumia reki ya ubao ili kuvuta udongo kutoka sehemu zilizoinuka kuelekea sehemu zilizo bondeni
6.VYANZO NA ATHARI ZA UPOTEVU WA MAJI YA UMWAGILIAJI
Ili kupata maji ya kutosha inabidi kuhakikisha kwamba upotevu wa maji ya umwagiliaji unapungua kwa kiwango kikubwa na wakulima wanamwagilia maji kwa kiasi kinachohitajika bila kuzidisha kiwango.
Vyanzo vya upotevu wa maji ya umwagiliaji katika skimu za mfano ni pamoja na:
• Maji yanayopotea kwenye mifereji mikuu, ya kati na ile midogo ya kusambaza maji mashambani.
• Maji yanayopotea mashambani wakati wa kumwagilia.
Upotevu wa maji kwenye mifereji mikuu, ya kati na ile ya kusambaza maji unasababishwa na aina ya udongo uliotengeneza kingo za mfereji, uchafu na matengenezo hafifu ya mifereji. Katika baadhi ya skimu upotevu wa maji kwenye mfereji mkuu uliosababishwa na kuvuja maji kwenye tuta la mfereji mkuu na kunywea chini ya ardhi ulikuwa mkubwa kiasi cha kuathiri upatikanaji wa maji kwenye mashamba yaliyoko mbali na banio.Vilevile athari nyingine ilikuwa ni maji mengi kuingia sehemu yasikohitajika na kusababisha tatizo la maji kutuama kwa muda mrefu.Hivyo wakulima wanashauriwa kupunguza upotevu huu wa maji kwenye mfereji kwa kujengea na kusakafia. Upotevu wa maji mashambani wakati wa kumwagilia unasababishwa na kuvuja kwenye tuta linalozunguka jaruba, kunywea chini na kuzidisha kiwango cha maji ya kumwagilia kinachotakiwa. Hii mara nyingi inasababishwa na utengenezaji mbovu wa jaruba. utengenezaji wa majaruba na uimarishaji wa kingo za jaruba umesaidia kupunguza upotevu wa maji kwa kiwango kikubwa na hatimaye kuongeza mavuno na kipato cha mkulima.
7. UPANDIKIZAJI MPUNGA
Ili kupata mavuno mengi na kukifanya kilimo cha mpunga kuwa cha faida ni muhimu wakulima kuzingatia mbinu hii muhimu na kuachana na kilimo cha kiholela kwa kumwaga mbegu moja kwa moja shambani. Aidha kwa wakulima wanaofuata kanuni hii wamepata mafanikio makubwa.
Faida zinazopatikana kwa kupandikiza mpunga
• Mkulima huweza kuchagua miche bora na mizuri ikiwa kitaluni.
• Miche hukua haraka na yenye afya .
• Kiasi kidogo cha mbegu huhitajika.
• Mavuno huwa mengi.
Njia za kupandikiza miche ya mpunga
Zipo njia kuu mbili za kupandikiza miche ya mpunga, nazo ni:
• Kupandikiza kwa mistari
• Kupandikiza bila ya kufuata mistari (Mchaka mchaka).
Aidha kati ya njia hizi mbili, njia ya kupanda kwa mistari ndiyo inayopendekezwa.zaidi. Pamoja na kwamba upandikizaji wa mistari unahitaji nguvu kazi zaidi, njia hii imeonyesha kuwa na mafaniko mengi ikilinganishwa na kupandikiza kiholela. Shamba lililopandwa kwa mistari ni rahisi kupalilia kwa kutumia kipalizi cha kusukuma kwa mkono. Pia ni rahisi kwa mkulima kupanga idadi ya mashina/mimea kwa eneo kwa uchagua nafasi aitakayo itakayompa mazao mengi.
Uandaaji wa miche
Kabla ya kupandikiza miche shambani ni muhimu kufanya maandalizi yafuatayo:
• Inashauriwa kumwagilia miche kwanza ili kupata urahisi wa kungo’a
• Ili kuzuia miche isikatike ovyo, miche ing’olewe kwa kushikwa chini zaidi ya shina
• Epuka kung’oa miche mingi kwa wakati mmoja
• Miche ifungwe kwenye mafungu madogo madogo ili kurahisisha usafirishaji na upandikizaji shambani
• Miche bora tu ndio ichaguliwe. Sifa za miche bora
• Iwe na kimo kinacholingana,
• Iwe na majani mafupi yaliyosimama, yenye mizizi mingi na yenye afya, isiyoshambuliwa na wadudu wala magonjwa,
Jinsi ya kupandikiza miche
• Miche ishikwe kwa vidole vitatu kama inavyoosha kweye picha chini
• Pandikiza kati ya miche 2 -3 kwa kila shina
• Kwa mafanikio zaidi, miche ipandikizwe katika kina cha sentimita 2-3
Continue »
NA SWATY BOY
VIJANA wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida wamehimzwa kuondokana na uvivu na badala yake waelekeze nguvu zao katika kilimo cha kibiashara cha viazi vitamu ili waweze kujikomboa kiuchumi.
Changamoto hiyo imetolewa na mkulima na mfanyabiashara wa zao la viazi vitamu na mkazi wa kijiji cha Nkuninkana,Ibrahimu Kilu (34) wakati akizungumza na MOblog juu ya kilimo hicho cha viazi vitamu ambacho pia ni zao la chakula.
Amesema kuwa zao la viazi vitamu ambalo miaka ya nyuma lilikuwa ni zao la ziada (halikupewa umuhimu unaostahili) hivi sasa zao hilo lina soko zuri ndani na nje ya nchi.
“Viazi vitamu kutoka wilaya yetu ya Ikungi vinakimbiliwa sana na wafanyabiashara kutoka mkoa wa Dodoma,Morogoro,Dar-es-salaam,Tanga na mikoa mingine nchini, pia kuna wafanyabiashara wanatoka Zambia na Comoro Kwa hali hiyo soko la zao hilo ni kubwa na linalipa vizuri”,alifafanua Ibrahimu.
Ibrahimu amesema toka aanze kulima zao hilo kibishara miaka mitano iliyopita limemwezesha kujenga nyumba bora na ya kisasa yenye choo ndani,amenunua pikipiki,anao mtaji wa kutosha na anasomesha watoto wake bila shida.
“Kilimo cha kibiashara cha viazi vitamu kina faida nyingi kinainua mhusika kiuchumi na pia uhakika wa kukabiliana na makali ya njaa unakuwepo.Mfano mzuri ni kwamba mimi msimu uliopita nililima uwele katika mashamba yangu yote na nilipata chakula cha kutosha kwa miaka miwili mfululizo”,amesema na kuongeza;
“Msimu huu,kwa sababu nina chakula cha kutosha mashamba yote nimelima viazi vitamu kwa lengo la kuboresha uchumi wa familia yangu matarajio ni kwamba natarajia kuingiza mapato ya zaidi ya shilingi milioni tatu”.
Akifafanua zaidi, Ibrahimu amesema faida ya kilimo cha viazi vitamu ni kwamba msimu huu nikilima mashamba yote viazi zao hilo la viazi hurutubisha ardhi kwa kiwango kikubwa na hivyo msimu ujao atakapolima uwele atakuwa na uhakika wa kuvuna zaidi ya lengo.
Wakati huo huo, wakulima hao wamelalamikia tabia ya wafanyabiashara kuwalazimisha kujaza viazi vitamu kwenye magunia aina ya rumbesa ambayo yana uzito wa zaidi ya kilo 130 ambao kisheria haikubaliki.
Kwa upande wake Afisa Kilimo na Mifugo wilaya ya Ikungi,Ayubu Sengo amesema wakulima wenyewe ndio wanaochangia biashara ya viazi vitamu ifanyike kwenye magunia ya rumbesa.
“Wakulima wetu kwanza ni watu wa ajabu kidogo na uvivu fulani upo ndani yao badala ya wao kuvuna viazi na kuvijaza kwenye gunia wao wanamwachia mnunuzi avivune kwa maana ya kuvichimba na kuvijaza kwenye magunia ya rumbesa na ndipo mkulima atalipwa kulingana na idadi ya magunia ya rumbesa”,alifafanua Sengo
Continue »
FIVE ADVANTAGE FOR MEN TO EAT WATER MELON[ FAIDA TANO AMBAZO UTAPATA MWANAUME UKILA TIKITI MAJI
9:46 AM 0 comments
INA need to describe the type of melon fruit (watermelon), of course, everyone knows, either to see or to eat it. But there are elaborations of the importance of its health benefits. Apart from being a rich source of Vitamin A, B6, C, 'Potassium' 'Magnesium' and other supplements tablet, this fruit also contains other nutrients capable of arousing feelings of physical (Sex libido) and eliminate the problems of loss of power male (Erectile Dysfunction).
as Viagra
Scientists say that Melon contains nutrients that can bring physical as emotional person pill table to add the power of the male Viagra. The fruit has shown soften well blood vessels and make mzunguruko blood count was slow without any adverse effects.
LIMITATIONS OF impotent and Sterility
According to scientists, Melon contains nutrient kind of 'arginine', which stimulates the production of 'Chemical oxide' the blood vessels thereby increasing sexual power as does the medicine Viagra.
Research surveyed 50 men who have problems with sexual power, showed that men were able to have sex after being given pills nutrition (food supplement) rich in B vitamins nourishment kind of 'arginine'.
strengthens mUSCLES
Foods high in mineral form of 'Potassium' such as Melon, strengthens the muscles of the body and greatly benefits the athletes. Eating a slice of Watermelon after doing intense exercise, it eliminates the problem of stretching the muscles of the legs.
Helps reduce body weight
Melon contains trace amounts of calories but contains a large amount of water, so for someone who wants to reduce body weight may help to eat in abundance which will be felt stomach full but would be satisfied too, so it easy to refrain from eating other foods even for a day and without compromised health.
Strengthens Immune
supplements of 'arginine' entailed in Melon depth much work the body, off some of the work outlined above, also stimulates significantly strengthening the immune system. As you know, the immune system is the foundation of good health, because with a strong immunity is not plagued by disease even one day.
Removes toxins from the body
'Arginine' also performs the important task of healing the wounds and remove 'ammonia' and other toxins from the body, persist causes a hearing fatigue and lead to liver disease and kidney.
OTHER BENEFITS
Benefits of Watermelon health are many, this fruit should be eaten by patients of hypertension as lowers pressure on the blood, increases light eyes, provides great protection against opportunistic infections including those risks such as cancer of the breast, bladder, lung and stomach cancer.
NOTE
Fruits like these should be eaten regularly and while you are grown to give immunity your body to fight disease themselves, do not wait until put to the disease and to be told doctor's start eating, always remember prevention is better than cure
Tunda hili limeonesha kulainisha vizuri mishipa ya damu na kufanya mzunguruko wa damu mwilini kuwa mwepesi bila athari yoyote mbaya. UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UGUMBA Kwa mujibu wa wanasayansi, Tikitimaji lina kirutubisho aina ya 'arginine', ambacho huchochea uzalishaji wa 'nitric oxide' kwenye mishipa ya damu na hivyo kuongeza nguvu za kiume kama ifanyavyo dawa ya Viagra. Utafiti waliofanyiwa wanaume 50 waliokuwa na matatizo ya nguvu za kiume, ulionesha kuwa wanaume hao waliweza kufanya tendo la ndoa baada ya kupewa vidonge lishe (food supplement) venye kirutubisho aina ya 'arginine'. HUIMARISHA MISULI Vyakula vyenye kiwango kingi cha madini aina ya 'Potassium' kama vile Tikitimaji, huimarisha misuli ya mwili na huwafaa sana wanamichezo.
Continue »

Most have been used as a vegetable or any one link in kunogesha vegetables but very few who know the health benefits of tomatoes painful.
With vegetables do have a taste and smell of its kind, bitter tomatoes have much work in the human body as well as to build and strengthen the health of consumers.
Tomato pot is in a group of vegetables have many nutrients, including vitamin A, B, and C which all together makes the task of kuobresha overall health of the body.
Tomato heap also helps strengthen the immunity of the flesh and help consumers avoid magonwja constant. These gloves are also turning away iayoweza eater heart disease. For patients with painful diabetic grandmother is also a drug that can help in reducing the level of sugar in the body.
Vitamin K is found in a heap of tomatoes helps to strengthen the blood vessels that support the whole process of blood circulation in the human body.
Despite being nearly 90 percent of tomato juice Mugu is this vegetable also contains iron and potassium
Continue »

Jina la kitalaamu la PILI PILI HOHO ni Capsicum annum. Asili ya zao hili ni bara la Amerika ya Kusini. Hapa nchini zao hili hulimwa katika mikoa ya Iringa, Tanga (Lushoto), Mbeya, Ruvuma, Tabora na Arusha.
Kilimo hiki kinaendeshwa na wakulima wadogo katika maeneo yenye ukubwa wa kati ya hekta 0.2-0.4 pia kuna maeneo ya wakulima wakubwa wenye hekta kati ya 2-20. Wakulima hao hujishughulisha na kilimo cha zao hilo kwa njia ya mkataba na kampuni hiyo.
Hoho hutumika katika kutengeneza rangi za asili za vyakula ambazo kwa sasa hupendwa zaidi kuliko zile zinazotokana na kemikali na pia huongeza ladha na harufu katika vyakula.
Hivyo hutumika katika viwanda vya kusindika vyakula, kwa mapishi ya nyumbani na hata katika viwanda vya vipodozi kama rangi ya mdomo, uso n.k. Ina virutubisho muhimu vinavyohitajika mwilini kama madini ya chuma, vitamin A na C.
2.0 TABIA YA MMEA
Hoho ni zao la jamii ya pilipili isiyo kali, tunda lake ni nene kiasi la duara pia linaweza kuwa lililochongoka,.
3.0 ENEO NA HALI YA HEWA INAYOFAA KWA KILIMO
Hoho hustawi vema katika maeneo ya usawa wa bahari hadi mwinuko wa mita 2,000 yenye mvua ya wastani wa mm.600-1,250 na wastani wa joto la nyuzi za sentigredi 21 hadi 24.
Udongo wa tifitifu wenye rutuba, usiotuamisha maji na wenye hali ya uchachu (pH) kati ya 5.0-6.5 hufaa zaidi. Umwagiliaji ni muhimu pale mvua inapokuwa chache.
4.0 UZALISHAJI
4.1 UTAYARISHAJI WA KITALU
Chagua eneo katika ardhi isiyo na mtelemko mkali na yenye rutuba ya kutosha. Ardhi iwe imepumzishwa bila kuoteshwa mazao ya jamii ya pilipili, biringanya, nyanya, n.k. ili kuepukana na mashambulizi ya wadudu na magonjwa.
Tayarisha kitalu kabla ya msimu wa mvua. Andaa vizuri matuta manne yenye urefu wa wastani wa mita 10 kila moja na upana wa mita moja (1) ili kustawisha miche inayotosha ekari moja.
Acha njia ya nusu mita kati ya tuta na tuta. Mwagilia maji ya kutosha siku moja kabla ya kusia mbegu na endelea kunyweshea kulingana na hali ya hewa na hali ya udongo.
Sia mbegu kwenye, mstari, nafasi kati ya mstari na mstari ni sm 10 na kina cha sm1. Kiasi cha mbegu cha nusu kilo kinatosha eneo la hekta moja.
Weka matandazo kwenye kitalu au tumia nailoni nyeusi ili kuhifadhi unyevunyevu na kuzuia uotaji wa magugu.
4.2 UTAYARISHAJI WA SHAMBA
Shamba lilimwe vizuri na kuweka matuta ili kuhifadhi unyevunyevu na kurahisisha umwagiliaji.
Matuta yanaweza kuwa makubwa au madogo kulingana na matakwa ya mkulima. Matuta makubwa hupandwa mistari miwili na matuta madogo hupandwa mstari mmoja.
4.3 UPATIKANAJI WA MBEGU
Mbegu ambazo hutumika ni chotara ambazo huuzwa kwenye maduka ya pembejeo za kilimo nchi nzima.
Haishauriwi kutumia mbegu kutoka zao la msimu uliopita kwani ubora wa paprika utaharibika na hivyo kuharibu soko unashauriwa kununua mbegu bora.
4.4 UPANDAJI
Mbegu huoteshwa na kukuzwa kitaluni kwa muda wa wiki 6-8 na miche hupandikizwa shambani ikiwa na urefu wa sm.6-10. Mwagilia maji kitaluni kabla ya kuhamisha miche.
Panda shambani kwa nafasi ya sm.75-90 kati ya miche kwa sm.90-105 kati ya mistari, wastani wa miche 12,500 itapatikana kwa hekta.
Weka samadi shambani tani 25-37 kwa hekta wiki 1-2 kabla ya kupandikiza miche, au kilo 560-670 za NPK (mbolea ya viwandani) kwa hekta kwa uwiano wa 4:7:7 katika udongo usio na rutuba ya kutosha.
5.0 KUHUDUMIA SHAMBA
Palizi ifanyike mara magugu yanapotokea shambani. Umwagiliaji maji ufanyike kama ilivyo kwa mazao mengine kama nyanya.
Tumia mbolea kiasi cha kilo 140 za SA au CAN kwa hekta hasa wakati mmea inapotoa matunda ili kupata matunda makubwa na kuvuna kwa muda mrefu (hadi miezi 10).
6.0 MAGONJWA NA WADUDU
Wadudu
• Funza wa vitumba
• Vidukari
• Kidomozi (Leaf miner)
Kudhibiti: Tumia dawa aina ya permethrin Magonjwa
• Kuoza mizizi
• Mnyauko wa majani
• Batobato
Kudhibiti: Choma nyasi kwenye kitalu kabla ya kusia mbegu.
Badilisha mazao yasiyo ya jamii ya pilipili.
7.0 UVUNAJI
Matunda ya kwanza huwa tayari kuvunwa kuanzia miezi 2-3 baada ya kupandikizwa; matunda yaliyokomaa vizuri na kuwa na rangi nyekundu ndiyo huvunwa. Matunda 30-80 hupatikana kwa mmea mmoja.
Ubora wa hoho huongezeka kutegemeana na kiwango cha rangi yake ikiwa ni nyekundu njano au kijani. Mazao kiasi cha tani 3.5 kwa hekta hupatikana.
Baada ya kuvuna mwagilia maji, piga dawa (kama ni muhimu) na weka mbolea kuongeza uzalishaji unaofuata.
8.0 USINDIKAJI
Hoho huuzwa ikiwa bado fresh tofauti na jamii nyingine za pilipili ambazo zinaweza kukaushwa na kusindikwa kasha kuuzwa baadae.
9.0 SOKO LA PAPRIKA
Soko la hoho lipo nchi nzima kwenya masoko makubwa na hata magengeni, hoho hutumiwa zaidi kama kiungo cha kupikia mapishi mbali mbali au kutia kwenye kachumbari.
Tatizo kubwa wanalokabiliana nalo wakulima ni kutokuwa na soko la uhakika ndani na nje ya nchi, mazao huweza kuoza shambani au njiani kutokana na tabu ya usafiri hasa vijijini ambapo mvua zikinyesha barabara hazipitiki kwa urahisi
Kuna aina ya pilipili isiyo kali kama hoho lakini ni ndefu kama pilipili za kawaida ijulikanayo kama PAPRIKA ambayo ina soko kubwa nje ya nchi.
Zao hili kwa sasa huzalishwa kwa msukumo wa kampuni ya kigeni ya Hispania inayoitwa Tanzania Spices Ltd iliyopo mkoani Iringa
10.0 GHARAMA YA UZALISHAJI WA HEKTA MOJA:
Mbegu Tshs. 24,000 /-
Vibarua 200,000/-
Mbolea(mboji/samadi) 300,000/-
Madawa 100,000/-
Jumla 624,000/-
MAPATO:
Kilo 3,500/- X 800/- 2,800,000/-
Continue »
Subscribe to:
Comments (Atom)








